
Ikiwa wewe ni mkaazi wa kaunti ya Kilifi, juwa kwamba sasa ni marufuku kukata miti nyumbani kwako bila idhini.
Naibu kamishna wa eneo Malindi- Thuo Ngugi, amewataka wakazi kupata leseni kutoka idara ya msisitu kabla ya kukata miti katika boma zao.
Kulingana na Thuo, hatua hiyo inalenga kupiga vita uharibifu wa mazingira kupitia ukataji miti kiholela.
Pia ameonya vikali wachomaji makaa akisema watakamatwa kwa kukata miti ovyo.