Wahudumu wengi wa matatu hapa Mombasa na pwani kwa ujumla wameonekana kususia kauli ya kurudi kazini.
Uchunguzi wa Baraka fm umebaini kuwa magari mengi bado yameegeshwa na kuwaacha abiria wakitembea kwa miguu kuelekea kwa shughuli zao.
Katika barabara ya Tudor, ni matatu mbili pekee yanahudumu sawia na Magongo na Bamburi.
Hapo jana muungano wa wamiliki wa matatu ulisitisha mgomo huo wa kupinga utekelezwaji wa sheria za Michuki.
Hayo yakijiri, nauli ya kufika mjini imepanda maradufu huku magari ya kibinafsi yakiitisha kati ya shilingi 150-hadi 200.