Raila ajipiga kifua kuwa atashinda kura ya urais

0
1170

Nairobi,KENYA:Muungano wa NASA umeeleza matumaini wa kushinda uchaguzi mkuu wa mwezi agosti.

Akizungumza katika mkutano wa kiaisa ulioandaliwa uwanja wa Bhukungu Kakamega, kinara wa muungano huo Raila Odinga amesema wataleta mabadiliko nchini iwapo watachukua uongozi wa nchi.

Wakati huo huo viongozi wa muungano huo wamekosoa serikali ya jubilee wakisema inaendesha nchi vibaya.

Viongozi waliohudhuria mkutano huo ni pamoja na Kalonzo Musyoka,.Musalia Mudavadi, Moses Wetangula, Charity Ngilu, na gavana wa Mombasa Hassan Joho.

Comments

comments