Mombasa,KENYA:Gari moshi mpya ya kisasa ya SGR itakuwa na uwezo wa kuwabeba abiria 1,200 kwa wakati mmoja.
Aidha safari ya gari moshi hilo itakuwa saa 5 kutoka Nairobi-Mombasa.
Shirika la reli nchini linasema kuwa safari ya kwanza ya SGR itakuwa tarehe 31 mwezi huu wa mei.
Mkurugenzi wa shirika hilo Atanas Maina amesema kutakuwa na safari moja kwa siku.
Rais Uhuru Kenyatta anatarajiwa kuzindua rasmi mradi huo.