Mombasa,KENYA: Mwanaume mmoja amefikishwa kortini Mombasa akishtakiwa kwa kosa la kumnajisi msichana wa miaka 13.
Felix Otieno Mito anadaiwa kutekeleza unyama huo katika mtaa wa Owino Uhuru eneo bunge Jomvu.
Lakini amekana mashtaka mbele ya hakimu mkuu Julius Nang’ea.
Ameachiliwa kwa dhamana ya shillingi laki tatu, huku kesi ikisubiri kutajwa tarehe 11 mwezi huu.