Mahakama yaagiza TV kurudishwa hewani

0
1282

Nairobi,KENYA:Mahakama imeondoa marufuku ya serikali dhidi vituo vya telvisheni kupeperusha matangazo.

Jaji Chacha Mwita pia ameagiza serikali kutohangaisha stehsni hizo.

Amesema agizo hilo litasalia hadi februari 14 ambapo kesi ambayo imewasilishwa kupinga hatua hiyo ya serikali kuskilizwa.

Mwanaharakati Okiya Omtata alienda kortini kutaka agizo hilo kuondolewa.

Waziri wa usalama wa ndani Fred Matiang’i alionya kuwa watu waliohusika na uapisho wa kinara wa Nasa Raila Odinga watakamatwa na kushtakiwa wakiwemo wenye vyombo vya habari.

Comments

comments