Dadake rais Uhuru Kenyatta, Margaret Wambui aaga dunia

0
1966
Margaret Wambui Kenyatta - PICHA: HISANI
Nairobi,KENYA: Dadake rais Uhuru Kenyatta, Margaret Wambui ameaga dunia.

Wambui ameaga dunia Jumatano akitibiwa Nairobi Hospital.

Wambui, amefariki akiwa na umri wa miaka 89.

Alikuwa mwana wa kike wa pekee na kifungua mimba katika familia ya hayati mzee Jomo Kenyatta na mke wake wa kwanza Nyokabi.
Marehemu Wambui pia alikuwa mwanamke wa kwanza muafrika kuwa Meya wa Nairobi. 

Hakuwahi kuolewa na hakuwa na watoto.

Comments

comments